Vyama 7 vya siasa Vyakutwa na Hati CHAFU

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Profesa Mussa Assad amesema kuna vyama saba vya siasa vimepata hati chafu baada ya kukaguliwa hesabu zake za mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha wa 2016/17.
Prof. Assad ameyasema hay oleo Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akikabidhi ya ukaguzi wa hesabu za serikali ya mwaka wa fedha ulioisha wa 2016/17 kwa Rais John Magufuli.
Miongoni mwa vyama vilivyotajwa ni pamoja na  chama cha Demokrasia Makini, TLP na ADC.
“…Chama cha Demokrasia Makini, Alliance for Democratic Change na Tanzania Labour Part, vyama saba vilivyopata hati chafu, sheria inatutaka sisi tukague vyama vya siasa, iwe vinapata ruzuku havipati ruzuku ni jambo lingine kwa namna hiyo tumetoa muhtasari wa vyama vya siasa,” Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Profesa Mussa Assad.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo