Wanafunzi wa kidato cha 6 ambao ndio wahitimu wakiingia Ukumbini
Wanafunzi hao wakisoma Risala
Mgeni rasmi akitoa hotuba yake
WANAFUNZI wa kidato cha sita katika
shule ya sekondari Lupalilo wilayani Makete mkoani Njombe wameeleza furaha yao
baada ya kusherehekea mahafali yao
ambayo ni ya tatu yaliyofanyika jana shuleni hapo
Wakizungumza nasi katika
sherehe za mahafali hayo shuleni hapo,
wanafunzi hao wamesema hatua waliyoifikia kwa sasa ni hatua nzuri katika
kuelekea kutimiza ndoto zao.
Aidha wameongeza kwa kuwaasa
wanafunzi wengine walio katika ngazi ya chini kuwa ili kufikia hatua yoyote
maishani jambo la msingi ni kuwa na jitihada na uvumilivu.
Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo
mwalimu Johnes Liombo amesema mwaka 2016
walipokea wanafunzi 215 ambapo wengine walihama na wanaotarajia kuhitimu kidato
cha sita ni zaidi ya wanafunzi 170, na kuongeza kuwa lengo la kufanya mahafali hayo mapema ni
kuhakikisha wanafunzi wanakuwa na muda wa kutosha wa kufanya maandalizi ya
mitihani yao ya mwisho.
Katika mahafali hayo mgeni alikuwa
ni kaimu mkuu wa TAKUKURU wilaya ya
makete Bw, Topela Kashinde ambapo naye
amesema serikali inafahamu fika changamoto zinazowakabili wanafunzi hao na ipo katika uangalizi mkubwa.
Wanafunzi wa kidato cha sita ndani ya mwezi wa tano mwaka huu
wanatarajia kufanya mtihani wa taifa ambao ni mtihani wao wa mwisho