Amzika mtoto wake akiwa hai

Polisi wa Migori nchini Kenya wanachunguza kifo cha mtoto mwenye umri wa miezi 6, ambaye inasemekeana alifukiwa akiwa hai na baba yake mzazi

Kwa mujibu wa kiongozi wa eneo hilo Chief Fredrick Owino, mwanaume huyo aliyetambulika kwa jina la Marcellus Odek, alirudi nyumbani kwake akiwa amelewa na kuchukua jembe na kuchimba kaburi, ambalo alimzika mtoto huyo ambaye ameelezwa alikuwa akisumbuliwa na tatizo la kupumua.
Taarifa zaidi zinasema kwamba mama wa mtoto huyo Annah Auma wakati tukio linatokea alikuwa amepoteza fahamu kutokana na tatizo la kifafa alilokuwa nalo, na alifanya tukio hilo mbele ya familia yake na majirani, usiku wa Machi 14 mwaka huu.
Ndugu wa familia hiyo Milicent Achieng amesema mtuhumiwa aliwakuta nyumbani na moto akiwa anapumua, kabla hjaanza kuchimba kaburi na kumfukia, na alipoomba msaada kwa watu walikataa nakumshauri akimbie kwani huenda angemuua na yeye.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo