Waziri: Natoa Wiki sita Tu

BWaziri wa nchi ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo ametoa wiki sita kwa Mkandarasi wa mradi wa maji Kivindo Wilayani Muheza kukamilisha mradi huo na uanze kutoa huduma kwa wananchi.
Waziri Jafo ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake Wilayani Muheza  ambapo alikagua miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo.
Alisema Mradi huo kwas asa umefikia asilimia 90 ya utekelezaji wake na Mkandarasi umeahidi hapa mbele ya wananchi kwamba utaukamilisha ndani ya muda niliokupa ambao ni wiki sita kuanzia hivi sasa.
“Sitegemei kuskia sababu zozote zitakazofanya mradi huu usikamilike ndani ya wiki sita ni mategemeo yangu wananchi wataanza kufaidi matunda ya mradi huu baada ya muda mfupi tu kuanzia sasa, Mkandarasi fanya kazi yako” Alisema Jafo.
Katika ziara hiyo Waziri Jafo amefanikiwa kutembelea Miradi ya afya na elimu katika kituo cha afya Mkuzi na Ubwari pamoja na kutembelea ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Msingi Kilulu. 
Waziri Jafo amewapongeza wadau mbalimbali wanaoshirikiana na Serikali katika ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika Maeneo ya Umma. Hususan ni Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMRI) kwa kutoa mifuko 50 ya Saruji kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa miundombinu katika kituo cha Afya Ubwari.
Halkadhalika Waziri Jafo ametoa wito kwa wadau wengine wa maendeleo kuendelea kushirikiana na Serikali katika kufanikisha ajenda ya maendeleo kwa wananchi.
Tamisemi ya Wananchi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo