TAKUKURU kumfikisha Mahakamani Kesho Kigogo wa UVCCM

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Dodoma imesema Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Sadifa Juma Khamis atafikishwa mahakamani kesho.
Kamanda wa Takukuru mkoani Dodoma, Emma Kuhanga amesema Sadifa atafikishwa mahakamani kesho Jumatatu Desemba 11,2017.
Amesema kiongozi huyo alikamatwa nyumbani kwake akiwapa soda wajumbe wa UVCCM kutoka Mkoa wa Kagera kitendo ambacho ni kinyume cha maadili.
UVCCM leo Jumapili Desemba 10,2017 inachagua viongozi wapya wa ngazi ya Taifa watakaoongoza jumuiya hiyo ya CCM kwa kipindi cha miaka mitano.
Sadifa ambaye pia ni mbunge wa Donge, Zanzibar amekamatwa nyumbani kwake Mailimbili mjini Dodoma.
Awali, Kuhanga akithibitisha kukamatwa kwa mwenyekiti huyo alisema, “Ni kweli tumemkamata tangu jana usiku tumekesha tunafanya uchunguzi, nitatoa taarifa baadaye kuhusu tukio hilo," amesema.
Chanzo:mwananchi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo