skip to main |
skip to sidebar
Rais Magufuli Ameagiza Kuondolewa kwa Bodi ya Umoja wa Vijana UVCCM
Mwenyekiti wa CCM, Dkt. John Magufuli ameagiza kuondolewa kwa Bodi ya Umoja wa Vijana UVCCM kwa maelezo kuwa haina tija.
-
Aidha, ameagiza mali zote za UVCCM ziandikwe kwenye daftari moja ili iwe rahisi kwa ufuatiliaji.
-
Amewataka pia vijana wa CCM wasiwe waoga na wanyonge katika kujibu hoja za wapinzani wao wa kisiasa.
-
Dkt. Magufuli ameyasema hayo leo mkoani Dodoma wakati akihutubia kwenye Mkutano wa 9 wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) ambao unafanya uchaguzi wa kuchagua uongozi mpya huku Mwenyekiti wa Umoja huo, Sadifa Khamis akiwa mikononi mwa Polisi kwa tuhuma za Rushwa.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi