Kikwete amtaja atakayempigia Kura awe Mwenyekiti wa CCM Taifa

Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) amefunguka na kusema kuwa anakwenda mjini Dodoma kwa ajili ya uchaguzi wa viongozi wa ngazi za juu wa chama

Ridhiwani Kikwete amedai kuwa kura yake kwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa itakwenda kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli 
"Ninakwenda Dodoma Kwenye Mkutano Mkuu kuchagua Viongozi wa Juu wa Chama Changu. Kura yangu ya Mwenyekiti nitamchagua Dr.John Magufuli.. Nakuomba nawe kura kwake" alindika Ridhiwani Kikwete 
Mkutano Mkuu wa Taifa wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) unatarajiwa kuanza Disemba 15, 2017 ambapo pamoja na mambo mengine watafanya uchaguzi wa viongozi mbalimbali wa ngazi ya juu ya chama hicho. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo