Rais Magufuli: Nimemwandikia barua waziri mkuu wa Canada kuhusu Bombadier Yetu

Rais John Magufuli amemwandikia barua waziri mkuu wa Canada kuulizia kuhusu ndege ya Bombadier, inayoshikiliwa nchini humo na kumtaka ashughulike suala hilo kwa haraka.

Akizungumza katika uzinduzi wa Uwanja wa ndege mjini Bukoba leo Jumatatu Novemba 6, Rais Magufuli amesema amemtuma pia Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju kwenda Canada kushughulikia suala hilo kisheria.

"Nimemwandikia barua waziri wa Canada kuulizia kwanini ndege yetu inakaa zaidi ya miezi sita, tumechoka kusubiri. Nimemtuma pia mwanasheria mkuu ili akapambane nao kisheria," amesema.

Amesisitiza kwamba kama wameamua kupambana kisheria watapambana na amewataka wanasheria wa Tanzania kushikamana ili kuhakikisha kwamba ndege hiyo inakuja Tanzania.

Rais Magufuli amewaonya wananchi pia kuacha kuzungumza kwenye mitandao ya kijamii. Alisema “ninawaomba watu wa vyama vyote waunge mkono juhudi hizi zinazofanywa na serikali.”

Magufuli ambaye ametimiza miaka miwili tangu achaguliwe kuwa Rais wa Tanzania amesema ndege zote sita zilizonunuliwa na Serikali zitakuja.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo