Mwanamke aliyefariki miezi 6 iliyopita afufuka Mwanza

Chausiku Miligo aliyedaiwa kufariki na kuzikwa miezi sita iliyopita, amezua taharuki kubwa baada ya kuonekana tena mtaani kwake Mbugani Kata ya Igoma, jijini Mwanza akiwa hai.
Majirani wa mwanamke huyo wameshangazwa na kitendo cha yeye kuonekana huku wakipigwa taharuki, kwani walithibitisha kifo chake na hata kuzikwa kwake.
Chausiku alipoulizwa mahali alipokuwa katika kipindi chote cha miezi sita alieleza kwamba alikuwa wilayani Bariadi, Mkoa wa Simiyu ambapo amemuacha mtoto wake wa kiume.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Mbugani alieleza kuwa Chausiku aliugua ghafla akiwa mjamzito na kupelekwa katika Hospitali ya Mkoa ya Seketule ambapo baada ya muda mfupi alifariki dunia na kisha taratibu za maziko zikafuatwa.
“Huyu mama aliugua na hatimaye akapelekwa katika hospitali ya mkoa ya Seketule, na baadae tulipata taarifa kuwa amefariki dunia na sisi kama mtaa tulifuata taratibu zote za kumsitiri. utaratibu wa maziko ulifanyika Shinyanga. Kwa hiyo tuliuaga na kutoa heshima zetu za mwisho na huyu mama alisafirishwa akapelekwa kuzikwa shinyanga,” alisema mwenyekiti wa mtaa wa Mbugani.
Umati wa watu ulikusanyika kushuhudia tukio hilo la aina yake ambapo kila mmoja alibaki akishangazwa kwa tukio hilo.
Familia ya Chausiku imeeleza kuwa ina mpango wa kumfanyia tambiko ili aweze kurejea katika hali yake ya kawaida.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo