AUDIO: Halmashauri ya wilaya ya Makete yapunguza Ushuru wa Mbao

 Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Mh Egnatio Mtawa (kulia) akitangaza mabadiliko hayo katika baraza la madiwani

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Mwl. Gregory Emannuel akizungumza jambo kuhusu mabadiliko hayo katika baraza hilo


Baraza la Madiwani Halmashauri ya wilaya ya Makete mkoani Njombe baada ya kupokea kero kutoka kwa wananchi, limekubali kufanya marekebisho ya sheria ya utozaji ushuru wa mbao kwa wilaya ya Makete

Hayo yamebainika katika Baraza la Halmashauri hiyo lililoketi hapo jana ambapo maamuzi hayo yamezingatia maoni mengi yaliyokuwa yakitolewa na wananchi kuhusu sheria hiyo


Mwanasheria wa Halmashauri Bw. Godfrey Gogadi ndiye aliyetoa taarifa ya Marekebisho hayo kwenye baraza la madiwani ambapo amesema ni jambo la kawaida kwa sheria kufanyiwa marekebisho na hakuna kosa lolote hapo na baadaye baada ya majadiliano na wajumbe wa baraza hilo maamuzi yakatangazwa na mwenyekiti wa halmashauri Mh Egnatio Mtawa

Akitangaza mabadiliko hayo Mh Mtawa amesema awali ushuru wa mbao uliokuwa unatozwa sh. 250 kwa ubao mmoja sasa utatozwa sh 150 kwa mbao laini na sh. 250 kwa mbao ngumu kuanzia alhamisi ya Novemba 23 huku akiagiza wataalamu wa halmashauri wanaohusika na mashine za kielektroniki za kutoza mapato wabadilishe viwango hivyo katika mashine zote

Sikiliza zaidi kwa kubofya play hapo chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo