Apanda mlima Kilimanjaro kwa baiskeli

Baada ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kuendelea kupanua wigo wa vivutio vya utalii katika Hifadhi zake 16 nchini, hatimaye aina mpya ya utalii imeweka rekodi ya kupanda mlima Kilimanjaro kwa baiskeli

Rekodi hiyo imewekwa na mpanda milima mashuhuri duniani kwa kutumia baiskeli Juanito Oiarzabal, ambaye amekuwa Mhispania wa kwanza kupanda Mlima Kilimanjaro kwa baiskeli akitumia saa 31 ndani ya siku tano hadi kufika kilele cha Uhuru.
Katika rekodi hiyo mpya Juanito aliambatana na wenzake wawili Eduardo Pascuaz na Ramon Abecia ambao walianza kupanda pamoja mlima huo mrefu kuliko yote barani Afrika kupitia lango la Kilema.
Kwa upande wake meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete amesema hatua hiyo ya Juanito na wenzake kufika katika kilele cha Uhuru ni ishara nzuri kwa aina hii mpya ya utalii katika Hifadhi za Taifa 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo