Dkt. Ndugulile amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akihojiwa na kipindi cha East Africa Breakfast, kinachorushwa na East Africa Radio wakati akielezea vipaumbele vyake mara baada ya kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa wizara hiyo hapo Oktoba. 7, na kuapishwa hapo jana
Naibu Waziri huyo amesema kuwa vipaumbele vingine ambayo atashirikiana na watumishi wingine wa wizara hiyo ni kuhakikisha anapunguza vifo vya kina mama na watoto pamoja kushughulia changamoto ya watumishi hasa maeneo ya pembembezoni.
Aidha ameongeza pia atashughulikia suala zima la kukamilisha mchakato wa Bima ya afya kwa wote kutokana na gharama za matibabu kwa sasa kuwa juu zaidi hivyo kwa kutumia bima itapunguza kwa kiasi kikubwa gharama hizo.
Dkt. Faustine Ndugulile amechukua nafasi ya Dkt. Hamisi Kigwangala baada ya Rais Magufuli kufanya mabadiliko katika baraza la mawaziri jumamosi iliyopita.