Wachache watatupinga - Humphrey Polepole

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Humphrey CCM, Polepole amefunguka na kusema watu wachache ndani ya nchi watawapinga kwa hisia na anasema anawahamasisha kuendelea kufanya hivyo lakini ukweli ni kwamba uchumi wa nchi unakuwa kwa kasi

Humphrey Polepole amesema hayo kupitia mtandao wake wa twitter alipoweka ripoti ya 'World Economic Forum' ambayo inaonyesha kuwa Tanzania ni kati ya nchi ambazo uchumi wake unakuwa kwa kasi kubwa barani Afrika, tofauti na hao watu wachache ambao wamekuwa wakipinga na kusema uchumi wa Tanzania haukuwi. 
Kufuatia bandiko hilo la Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole baadhi ya watu wameendelea kupinga kwa kusema hali ya maisha mtaani ni ngumu huku wengine wakidai huo uchumi unaosemekana kukuwa Tanzania hauna uhalisia na maisha ya kawaida ambayo watu wanaishi. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo