AUDIO: "Unyama" wanaoufanya wafanyabiashara wa Tandala Makete kwa Wateja

Wafanyabiashara wa kata ya Tandala wilayani Makete mkoani Njombe wametakiwa kutambua soko huria la kufanya biashara hivyo kuacha kasumba ya kuwaandama wafanyabiashara wanaofanya biashara zao kwa kuamua kupunguza bei

Akizungumza na wafanyabiashara hao hii leo, Diwani wa kata ya Tandala Mh Egnatio Mtawa amesema mara nyingi serikali inawaacha wafanyabiashara wafanye bishara zao kwa uhuru lakini pale wanapolazimika kuuza bidhaa kwa kiwango kilichopitiliza serikali haitasita kuingilia kati

Amesema katika siku za hivi karibuni amepokea malalamiko ya baadhi ya wafanyabiashara wanaouza bidhaa kwa bei ya chini kuandamwa na wafanyabiashara wengine kwa madai kuwa wanawaharibia soko, jambo ambalo amelikemea na kutaka kila mfanyabiashara auze bidhaa zake kwa bei anayoona inafaa lakini isipitilize kiwango cha juu kilichopendekezwa na serikali

Baadhi ya wananchi waliozungumza na mwandishi wetu baada ya kusikia yaliyojiri kwenye mkutano huo baina ya diwani na wafanyabiashara wametoa maoni yao

Katika hatua nyingine Diwani Mtawa amewataka wananchi kuchangamkia fursa pindi itakapojengwa kambi kwa ajili ya wakandarasi wanaotengeneza barabara ya lami kutoka Makete kwenda Njombe huku akiwaonya wafanyabiashara kununua bidhaa za wizi ama za magendo ikiwemo mafuta na saruji kuacha suala hilo kwa kuwa ni kinyume cha sheria na endepo wakibainika watachukuliwa hatua

Pia amewataka wafanyabiashara kuacha kufanya udanganyifu kwenye biashara zao kwa kigezo cha kulipa mapato madogo kwa mamlaka ya mapato nchini TRA


Sikiliza zaidi sauti hizi hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo