Kamishna wa Polisi Kanda Maaalum ya Dar es Salaam Simon Sirro amesema kuwa Jeshi hilo bado lipo kwenye upelelezi kuhusiana na kuvamiwa kwa Clouds Media Group na Mkuu wa Moa wa Dar es Salaam Paul Makonda na pindi upelelezi utakapokamilika hatua zinazotakiwa zitafuata ikiwa ni pamoja na kulifikisha jalada kwa Wakili wa Serikali.
Kamanda Sirro amesema hayo mbele ya wanahabari ambao walihoji hatua ambayo upelelezi huo ulipofikia na namna jambo hilo linavyoshughulikiwa: “Kesi ni ushahidi Kwa hiyo ndugu zetu bado tunapeleleza lakini niwaombe ndugu zetu wa Clouds waendelee kutupa ushirikiano, watupe ushahidi…mimi kazi yangu ni kupeleleza…nikishapeleleza ushahidi uliopo napeleka kwa Wakili wa Serikali.” – Kamanda Sirro.