skip to main |
skip to sidebar
Njiwa aliyesafirisha dawa za kulevya akamatwa
Polisi wa Kuwait wamemkamata njiwa aliyekuwa amebeba dawa za kulevya aina ya Ketamine ambaye alikuwa amenasa kwenye bati la jengo la forodha katika Bandari ya Abdel iliyopo mpakani mwa Kuwait na Iraq.
Katika taarifa iliyoripotiwa na BBC njiwa huyo alikamatwa baada ya kushindwa kuruka baada ya kuzidiwa na uzito wa dawa hizo ambapo alikuwa amebebeshwa kibegi kidogo mgongoni kilichojazwa vidonge 178 vya dawa zinazoaminika kuwa na thamani kubwa akidaiwa kutoka Iraq.
Mbinu hii ya kutumia njiwa katika kusafirisha dawa za kulevya imekuwa ikitumika sana kwenye sehemu zenye ulinzi mkali ambapo mwaka 2015 iliripotiwa kukamatwa kwa njiwa aliyebeba dawa za kulevya aina ya Cocaine na Bangi katika ukuta wa jengo la gereza Costa Rica.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi