Na Omary Mngindo, Chalinze
MKAZI wa Kitongoji Magwila Kata ya Bwilingu Halmashauri ya Chalinze, Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani Fatuma Ramadhani (32), anashikiliwa na jeshi la Polisi kwa tuhuma za kujifungua kitoto jinsi ya kike cha miezi 6 kisha kukifukia kwenye shimo.
Mtuhumiwa Fatuma Ramadhani
"Nimepigiwa simu na mmoja wa wakazi akinijuza kuhusiana na tukio hili la mwanamke kujifungua kisha kuchimba shimo dogo kukifukia, nikiwa mjumbe wa nyumba kumi nimejulishwa kutokea kwa tatizo hili, nikampigia Mwenyekiti wa Kitongoji naye akatoa taarifa Polisi na kwa Mganga Mkuu wa Kituo cha afya cha Bwilingu," alisema Mwanamosi.
"Nitoe wito kwa wanawake kujiunga na uzazi wa Mpango, hatua hii itasaidia kuwawezesha kujipangia uzazi watakavyo ukilinganisha na matukio kama haya yanayosababisha mlengwa kufanya tukio la kuua kitoto," alisema Dkt. Waziri.
Mwenyekiti wa Kitongoji Said Halfan alisema kwamba alijulishwa kutokea kwa tukio hilo, alifika eneo la tukio kushuhudia hali hiyo kisha akatoa taarifa kwa Mkuu wa Kituo cha Polisi na Mganga Mkuu wa Kituo cha Bwilingu ili kuanza kufuatilia taratibu za kitaalamu.
"Kama unavyoshuhudia askari na mganga wapo hapa kwa taratibu za kitaalam, baada ya taratibu tumeambiwa tukihifadhi hapahapo hiki kiumbe, tukio limenisikitisha sana, nitumie fursa hii kuwaomba wanawake kuacha tabia ya kutoa mimba au kuuwa viumbe kama mkazi huyu," alisema Halfani.
Akizungumza na mwandishiwa habari, Fatuma alusema kwamba ilipofika saa 11 alfajiri alianza kujisikia maumivu makali kabla ya kujifungua kwa bahati mbaya na kwamba huo ni uzazi wake wa tatu.
"Hii hali hata mimi imenishtua kwa sikutarajia kukutwa na tukio kama hili, ghafla nikiwa ndani ya chumba nikajisikia maumivu makali wakati nataka kuita wapangaji wenzangu ghafla nikajikuta nimejifungua," alisema Fatuma.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Onesmo Lyanga amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kwamba uchunguzi zaidi wa tukio hilo unaendelea kabla ya kufikishwa mahakamani.



