Chanjo ya watoto Makete, Ujumbe Mzito watolewa Kwa Wazazi

Wazazi na walezi wilayani Makete mkoani Njombe wameshauriwa kujitokeza kwa wingi kuwapatia chanjo watoto wao katika maadhimisho ya wiki ya chanjo duniani

Akizungumza na mwandishi wetu ofisisni kwake, Mratibu wa shughuli za Chanjo katika halmashauri ya wilaya ya Makete Bw. Felician Chawala amesema kiwilaya maadhimisho hayo yatafanyika katika kijiji cha Ndulamo kata ya Iwawa wilayani hapa kuanzia Aprili 24 hadi Aprili 30 mwaka huu huku mgeni Rasmi akitarajiwa kuwa Mkuu wa wilaya ya Makete

Amesema wilaya ya Makete haiko nyuma katika utekelezaji wa maadhimisho hayo na kusema wamejipanga kikamilifu kuhakikisha maadhimisho hayo yanafanyika kama ilivyopangwa

Bw. Emilian Mbijima ni Mratibu wa afya ya uzazi na mtoto Halmashauri ya wilaya ya Makete amesema ni muhimu kwa wazazi wote wawili baba na mama wakatambua umuhimu wa mtoto kupatiwa chanjo, hasa baba kwa kuwa itasaidia kumkumbusha mama pale anapokuwa amesahau wakaongozana kwa pamoja kumpeleka mtoto wao kupatiwa chanjo

Amesema ni furaha kwao wataalamu wa afya kuona jamii inaelewa umuhimu wa chanjo kwa watoto kwa kuwa inasaidia kuwakinga na maradhi mbalimbali pamoja na kuepusha vifo ambavyo vingetokana na watoto kutopatuiwa chanjo


Maadhimisho hayo yanaongozwa na ujumbe usemao "Chanjo hukinga kila mtu, pata chanjo" huku kaulimbiu ya mwaka huu ikisema "Jamii iliyochanjwa ni jamii yenye afya"


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo