AUDIO: Baada ya Bomoabomoa, DC Makete aweka wazi Lami ya Makete Njombe

Mkuu wa wilaya ya Makete Mh Veronica Kessy amewaomba wananchi wa wilaya hiyo kujitokeza kwa wingi kuupokea mwenge wa uhuru unaotarajiwa kuwasili wilayani hapa Mei Mosi mwaka huu

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu huyo wa wilaya amesema maandalizi ya kuupokea mwenge wa uhuru kwa mwaka huu 2017 yanaendelea vizuri ambapo mwenge huo unatarajiwa kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo, sanjari na kuungana na wafanyakazi katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani ambavyo vyote vitafanyika siku moja

Mh Kessy amesema mwenge huo utapokelewa eneo la Kimani katika kata ya Mfumbi ukitokea wilaya ya Wanging'ombe na kuwaomba wananchi kujitokeza katika maeneo yote utakakopita sambaba na eneo la Mkesha ambapo ni stendi ya Iwawa Makete mjini

Aidha mkuu huyo wa wilaya amezungumzia umuhimu wa kutunza mazingira hasa vyanzo vya maji, ambavyo vimekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wa Makete pamoja na maeneo jirani yanayotegemea maji kutoka wilayani Hapa

Hata hivyo amewapongeza wananchi wa Makete kwa kubomoa kwa hiari nyumba zao zilizokuwa zimejengwa kwenye hifadhi ya barabara, kupisha ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami toka Njombe hadi Makete, na kuwaomba wananchi kuendelea kuwa na subira licha ya kusikia ahadi za ujenzi wa barabara hiyo kwa muda mrefu bila kutekelezwa, lakini sasa muda wa utekelezaji umewadia

>>>Bonyeza Play hapo chini uweze kumsikiliza


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo