Majambazi wateka Magari matano na Kupora Fedha Kibiti

Kibiti. 

Watu sita wanaosadikiwa kuwa majambazi wakiwa na silaha wameteka magari matano na kupora Sh920, 000 na simu saba za mkononi katika eneo la Kitembo nje kidogo ya mji wa Kibiti.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga alisema tukio hilo lilitokea juzi saa moja usiku na kwamba abiria walioporwa walikuwa wakisafiri kwenye barabara itokayo Dar es Salaam kwenda Mtwara.

Aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni Issa Juma, Nassoro Mohammed, Kassim Omari, Issa Juma na Khalifa Mohammed, wote wakazi wa Dar es Salaam. Wengine waliojeruhiwa ni Badru Uwesu mkazi wa Kisemvule, Mkuranga na Edward Safari, mkazi wa Morogoro.

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mchukwi walikopelekwa majeruhi, Dk Japhet Guzuye alisema walikuwa na majeraha shavuni, migongoni na shingoni na walitibiwa na kuruhusiwa kuondoka.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo