Kijana aliepotea akutwa ndani ya tumbo la chatu akiwa amesha kufa

Mtu mmoja alie julikanwa kwa jina la Akbar  ambaye alikuwa ametoweka nyumbani kwa masaa kadhaa amekutikana akiwa amekufa ndani ya tumbo la chatu.
kwa mujibu wa polisi Akbar alitoweka siku ya Jumapili katika kisiwa cha Sulawesi, baada ya kuondoka nyumba akienda kuvuna mawese katika shamba la familia yao.
Mashura ambaye ni msemaji wa polisi katika mkoa wa Sulawesi Magharibi  aliiambia BBC, kuwa wanavijiji waliripoti kwa polisi kuwa Akbar hajaonekana kwa muda wa saa 24 Kisha polisi walianza kumtafuta nakugundua kuwa amemezwa na chatu huyo.
Chatu huyo ambae ana urefu wa mita saba alipopasuliwa tumbo, mwili wa mwanamume huyo ulipatikana ndani.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo