Ijumaa iliyopita kituo cha Clouds kilivamiwa na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akiwa na askari wenye mitutu kitendo kilichopingwa na wadau mbalimbali wa habari.
“Kesho Tarehe 23/03/2017 Saa nne kamili asubuhi, nitatembelea Ofisi za EFM na TVE ili kuwapa pole wana tasnia ya Habari kwa yaliyotokea.” aliandika mchungaji huyo kupitia ukurasa wake wa Instagram.
Askofu huyo leo alitembelea kituo cha Clouds kwaajili ya kutoa pole kwa yaliyotokea.
Na Emmy Mwaipopo
