AUDIO: Viongozi wa Mabaraza ya Kata Makete Waongezewa Ujuzi

 Washiriki wakifuatilia mafunzo hayo



Mwanasheria wa wilaya ya Makete Godfrey Gogadi akitoa elimu kwa washiriki

Serikali wilayani Makete Mkoani Njombe imeanza kutoa elimu kwa viongozi wa mabaraza ya kata juu ya utendaji kazi wa mabaraza hayo pamoja na vyombo vingine katika katika vijiji na kata.

Akizungumza Mwanasheria wa halmashauri ya wilaya ya Makete Bw.Godfrey Gogadi katika ukumbi wa Shirika la SUMASESU uliopo kata ya Tandala amesema lengo la mafunzo hayo ni kutoa maelekezo na kufundisha utendaji kazi wa mabaraza ya kata ambapo wamekutanishwa watendaji wa vijiji,watendaji wa kata, wenyeviti wa vijiji na viongozi wa mabaraza ya kata pamoja na wasaidizi wa kisheria.

BW.Godfrey amewataka viongozi hao kuyaishi yale waliyofundishwa katika mafunzo hayo na pale inapotokea inahitajika ushauri katika maamuzi ni vema wakatafuta washauri kwani nia ya serikali ni kuona mabaraza ya kata ya wilaya makete yanatenda haki.

Pia amewataka wananchi kuyatumia mabaraza ya kata kwa kutoa malalamiko yao ili waweze kutafutiwa suluhisho la malalamiko yao.


Mafunzo hayo yamewakutanisha viongozi kutoka tarafa ya lupalilo ikijumuisha kata ya Tandala ,ukwama mang'oto na Lupalilo

Msikilize Mwansheria huyo akizungumza:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo