Akizungumza wakati wakipatiwa fedha kiasi cha shilingi million 64 kutokana manispaa ya Temeke kwa ajili ya mitaji ya biashara ya ujasiliamali kwa vikundi 51 vya watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi manispaa ya Temeke,M/kiti wa mtandao wa watu wanaishi na VVU Said Kambangwa anaeleza.
Katibu tawala wa manispaa ya Temeke Hashim Komba amewataka watu wanaishi na VVU wasikate tamaa kwa kuwa halmashauri hiyo kwa kushirikiana na ofisi ya mkurugenzi itahakikisha inawasaidia kwa hali na mali ili kuimarisha afya zao lakini pia kuendesha biashara na ujasilimali ili kuongeza kipato kwa ajili ya kujikimu kimaisha.
Aidha Vikundi hivyo vya watu wanaoishi na VVU wamependekeza kuundwa Mfuko wa Taifa wa Ukimwi- Aids Trust Fund kuanzia ngazi ya kata,wilaya hadi mkoa ambapo vikundi hivyo katika wilaya ya temeke vina jumla ya wanachama wanawake 1260 na wanaume 480.