Mume apewa Kipigo na Mkewe Hadharani huko Moshi

Mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la Mama Tundu amempa mumewe kichapo na kumjeruhi usoni akimtuhumu kutoacha matumizi ya nyumbani.

Tukio hilo lililovuta umati wa watu lililitokea jana saa 2:00 asubuhi mtaa wa Msaranga Wilaya ya Moshi, baada ya mwanamke huyo kumtuhumu mumewe, Fredrick Masawe kutotoa fedha za matumizi.

”Nimechoka na tabia yake ya kunywa pombe kila wakati wakati sisi tunalala njaa kisa eti fedha zote anatumia baa na wanawake wake, siwezi vumilia leo mpaka kieleweke,'' alidai mwanamke huyo.

Akizungumza na gazeti hili baada ya kuamuliwa, mumewe alikanusha kuwa na wanawake bali mara nyingi huwa na marafiki wanaofanya kazi pamoja na kwamba pombe hizo hununuliwa na marafiki zake.

Chanzo: Mwananchi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo