AUDIO: Katikakatika ya Umeme, Makete yataka Umeme wa Gridi ya Taifa Utoke Moronga na si Mbeya

Serikali imeshauriwa kuangalia uwezekano wa kuhakikisha umeme wa gridi ya taifa unaotumika ndani ya wilaya ya Makete unatoka ndani ya Mkoa wa Njombe badala ya Mbeya ili kuepuka adha ya umeme huo inayowakumba wananchi endapo matatizo yanajitokeza kwa mkoa wa Mbeya

Kauli hiyo imetolewa Mkoani Njombe na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Mh Egnatio Mtawa katika kikao cha RCC mkoa ambapo amesema wananchi wa Makete mara nyingi wamekuwa wakikosa huduma ya umeme mara kwa mara kutokana na matataizo yanayojitokeza kwenye miundombinu ya TANESCO Mkoa wa Mbeya hivyo utatuzi wake umekuwa Mgumu kutekelezeka kwa wakati

Kisha Mh Mtawa akatoa pendekezo kwa serikali ni nini kifanyike ili kuondoa changamoto hiyo inayowakabili wananchi wa Makete wanaotegemea umeme wa gridi ya taifa

Katika hatua nyingine kupitia kwa mwenyekiti huyo halmashauri ya wilaya ya Makete imelalamikia gharama kubwa za matengenezo ya magari zinazotozwa na wakala wa serikali TEMESA, ambapo halmashauri hiyo magari iliyokuwa ikilipia shilingi laki 8 kwa matengenezo kwa sasa wanalazimika kulipia ZAIDI ya milioni 3 kwa TEMESA

Hali hiyo ikamlazimu aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi kutaka maelezo ya suala hilo kutoka TEMESA

Majibu hayo  yakapelekea aliyekuwa mkuu wa Mkoa wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi ambaye kwa sasa amehamishiwa mkoa wa Singida kutoa kauli kuhusiana na hilo


 Sikiliza sauti hizi hapa chini


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo