AUDIO: Amri ya Kutumia Stendi Mpya ya Tandala Makete Yapamba moto


Katika kuhakikisha stendi mpya ya Tandala katika wilaya ya Makete mkoani Njombe inaendelea kutumiwa na vyombo vya usafiri pongezi zimetolewa kwa wamiliki wa vyomo vya usafiri hususan Mabasi ya abiria kwa kuanza kuitumia stendi hiyo.

Akizungumza nasi Mwenyekiti wa kijiji cha Tandala Bw Andowisye Memba ametoa pongezi hizo kwa kusema kuwa ushirikiano wanaoutoa ni mzuri na kuwataka wasafiri kutambua kuwa kwa sasa stendi iliyopo katika kitongoji cha Singida, ndiyo inayotambulika rasmi na inaendelea kufanya kazi.
Aidha amewatoa wasiwasi abiria watakaoshukia katika stendi hiyo Kwa kusema kuwa watapata usafiri mwingine wa pikipiki hivyo waendelee kuitumia stendi hiyo.

Pia ameongeza kuwa kwa sasa hawatatumia kituo kingine kushusha  abiria mbali na stendi mpya ya Tandala.

na Asukile Mwalwembe
sikiliza sauti hapo chini kwa kubofya play


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo