Mwanafunzi akamatwa akitoa Mimba

Mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Matala wilayani hapa amekamatwa na polisi kwa madai ya kutoa mimba.

Kamanda wa Polisi Mkoa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa amesema jana kuwa mwanafunzi huyo na mshirika wake wanatarajiwa kufikishwa mahakamani upelelezi ukikamilika.

“Tunamsaka kijana aliyempa mimba na atakapopatikana sheria itafuata mkondo kwa kumfikisha mahakamani,” amesema.

Mbali na mwanafunzi huyo aliyelazwa Hospitali ya Kilema, pia jeshi hilo linamshikilia mama yake mdogo kwa madai ya kumsaidia kutekeleza kitendo hicho.

Babu wa mwanafunzi aliyetoa mimba, Henry Kaale amelalamika kushikiliwa kwa wanafamilia wakati mtuhumiwa muhimu hajakamatwa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo