Mkuu wa Shule akiona Cha Mtema Kuni.......Kisa Sare za CCM

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kasamwa ya mkoani Geita, Dennis Otieno anadaiwa kushushwa cheo kutokana na kuzuia wanafunzi kuvaa sare za CCM kwenye mahafali ya kidato cha nne.

Pia, taarifa hizo zinasema mkuu huyo wa shule alipinga kitendo cha baadhi ya walimu kuchangisha fedha wazazi wa watoto ambao ni wanachama wa Klabu ya Magufuli ili kufanya sherehe hilo kutokana na agizo la Rais la kufuta michango yote mashuleni.

Otieno, ambaye alikataa kuzungumzia suala hilo, anadaiwa kushushwa cheo kutokana na shinikizo la makada wa chama hicho tawala, hasa mwenyekiti wa CCM mkoani Geita, Joseph Kasheku, maarufu kwa jina la Msukuma, ambaye amethibitisha kushushwa cheo kwa mtumishi huyo wa umma.

Kwa mujibu wa taarifa hizo zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zinasema Otieno aligombana na mwalimu ambaye ni mlezi wa Klabu ya Magufuli kutokana na kuandaa mahafali hayo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo