Mbunge wa jimbo
la Makete mh. Prof. Norman Sigala King amekanusha tuhuma zilizotangazwa na vyombo vya habari na mitandao ya kijamii Dhidi yake kuwa
alikuwa bado akipokea mshahara wa ukuu wa wilaya kwa muda wa miezi mitano baada ya kuchanguliwa kuwa mbunge.
Amesema hayo leo hii wakati
akizungumza na kituo cha 91.5 Green FM katika mahojiano Maalum na kusema kuwa taarifa hizo
hazina ukweli wowote na kuwa serikali hii ya awamu ya tano ipo makini haiwezi
kuingiza mshahara huo wa ukuu wa wilaya katika akaunti yake wakati ikijua kuwa
yeye ni mbunge kwa sasa.
Mh. Norman pia
ametoa wito kwa vyombo vya habari kutotangaza taarifa hiyo bila kumhoji ili kuthibitisha tuhuma hizo huku akiwataka wananchi wa Makete kuendelea kufanya kazi ili kuijenga Makete na
kuwa yeye kama mbunge wao yuko makini.
Pia Mbunge huyo amesema hakuhojiwa na mwandishi wa gazeti la Mwananchi kama lilivyoandika na tayari ameshafika kwenye ofisi za Gazeti hilo kwa hatua zaidi
Bonyeza play hapo chini Kusikiliza mahojiano hayo kwa njia ya sauti:-