Wanafunzi hao wa darasa la mwaka wa tisa katika shule yaLonghill eneo la
Rottingdean, Sussex Mashariki, walikuwa miongoni mwa wanafunzi 20
wavulana waliovalia kaptura za kuvaliwa wakati wa mazoezi badala ya
suruali ndefu.
Baadhi walifukuzwa shuleni Jumanne na wengine kutengwa hadi siku
iliyofuata. Waliokubali kuvua kaptura hizo na kuvalia suruali ndefu
hawakuadhibiwa.
Lakini badala ya kuvalia sare kamili ya wakati wa masomo, kama
walivyokuwa wameagizwa, wanafunzi wanne walirejea shuleni Alhamisi
wakiwa wamevalia sketi.
Mwalimu mkuu Kate Williams aliwaambia wanaweza kuvalia mavazi yoyote, mradi yawe ni sehemu ya sare iliyokubalika shuleni.