Serikali yatangaza kuyafutia usajili magazeti 473

Kutokana na kuonekana kushindwa kutoa magazeti katika kipindi cha miaka mitatu, serikali imetangaza rasmi kuyafutia usajili magazeti 473 kutokana na kushindwa kutoa nakala katika kipindi cha miaka hiyo mitatu.

Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Nnauye amesema kuwa wamiliki wa magazeti hayo wamevunja sheria na kwa mujibu wa kifungu 23(1) cha Sheria ya Magazeti ambacho kinampa mamlaka ya kuyafutia usajili, anayafungia magazeti hayo.

“Kuna magazeti yana miaka mitatu sasa bado hayajatolewa nakala mengine yalikuwa yanatoa na baadae yakaacha na mengine hayajatoa kabisa, haya yote natangaza kuanzia leo yamefutwa usajili wake,” alisema Waziri Nape.

Waziri Nape alisema kuanzia sasa hairuhusiwi kwa mtu yoyote kuchapisha nakala za magazeti yaliyofungiwa na kwa kufanya hivyo atakuwa amekiuka Sheria ya Magazeti sura ya 229, kifungu cha 6 na hivyo atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Aidha Waziri Nape aliongeza kuwa kama kuna mmiliki wa magazeti ambayo yamefungiwa angependa kuendelea kuchapisha nakala za gazeti lake, milango ipo wazi kuwasilisha maombi mapya ya usajili kwa kufuata sheria zilizopo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo