PICHA: Watu 29 wapoteza maisha katika ajali ya mabasi ya City Boy, Rais Magufuli aguswa

Ajali mbaya imeyohusisha mabasi mawili ya kampuni ya City Boy imetokea katika kijiji cha Maweni wilaya ya Manyoni, Singida na kusababisha watu 29 kupoteza maisha papo hapo huku chanzo cha ajali kikitajwa kuwa ni mwendo kasi.

Mabasi hayo yenye namba za usajili T531 DCE na T247 DCD, moja lilikuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Kahama na lingine likitokea Kahama kuelekea Dar es Salaam.

Moja ya mashuhuda wa ajali hiyo amesema kuwa madereva wa mabasi yote walikuwa katika mwendo kasi na wakati ajali inatokea walikuwa wakisalimiana kwa kunyosheana mikono kisha basi moja kupoteza mwelekeo na kuingia upande wa basi lingine na ndipo yakakutana uso kwa uso na kusababisha ajali hiyo.

Kamanda wa Polisi Singida, Thobias Sedoyeka tayari amethibittisha kutokea ajali hiyo na uchunguzi zaidi unaendelea kufanyika.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli ametuma salamu za rambirambi na kueleza kuwa amepokea taarifa hiyo kwa mshtuko na amesikitishwa na ajali hiyo ambayo imechukua maisha ya watanzania.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo