Picha 11, Wananchi Utweve Makete watangaza Mgomo, Kisa Mauaji


Shughuli za kimaendeleo katika kijiji cha Utweve kata ya Ukwama wilayani Makete mkoani Njombe kuanzia jana zimesimama Kwa muda usiojulikana huku wananchi wa kijiji hicho wakihitaji hatma ya watuhumiwa wa mauaji ya mtoto mmoja wa kijiji hicho



Hayo yamekuja kutokana na kuanza kujadili Ajenda za mkutano juu ya ujenzi wa Zahanati kijijini hapo ndipo wananchi hao wakapinga kujadili Ajenda hiyo badala yake wakataka wapate mrejesho wa kinachoendelea juu ya watuhumiwa wa mauaji waliowekewa dhamana kama wamekamatwa ama lah kufuatia maazimio waliyowekeana kwenye mkutano uliofanyika Juni 22 mwaka huu.



Wananchi hao wamesema hawapo tayari kufanya shughuli zozote za maendeleo mpaka wapate hatma ya suala hilo


Pia wameweka wazi kuwa katika mkutano uliopita uliofanyika kijijini hapo Juni 22 mwaka huu ulimalizika salama na haukuwa na vurugu yeyote kama inavyodaiwa kuwa wapo wananchi waliofanya vurugu



Baada ya majadiliano ya muda mrefu wananchi hao wameazimia kuwa wanahitaji mkuu wa wilaya ya Makete afike kijijini hapo na viongozi wengine wa wilaya ili wasikilize kilio chao.



Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho Bw Rauteli Sanga amewaomba wananchi pamoja na wafiwa kuwa na uvumilivu wakati wananendelea na ufuatiliaji wa suala hilo la mauaji wakati vyombo vya dola vikilishughulikia kwa upande wao.











JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo