Makubwa: Wananchi wa Makete watishia kuchoma magari ya wawekezaji


Mgogoro wa ardhi katika mashamba ya Ludodolelo wilayani Makete mkoani Njombe umechukua sura mpya baada ya wananchi kutaka kuchoma magari ya wawekezaji na kuziba barabara huku wakitishia kuvamia mashamba hayo na kugawana baada ya viongozi wao kuzuiwa kuingia kwenye ukumbi wa kijiji wakati wawekezaji wakihojiwa na Tume iliyoundwa kuchunguza mgogoro huo. 

 Hatua hiyo imekuja baada ya diwani na mtendaji wa kata ya Mbalache wilayani Makete mkoani Njombe kutoruhusiwa kuingia kwenye ukumbi wa kijiji wakati wawekezaji wa shamba la Ludodolelo kampuni ya Silver lands na Kanisa Katoliki Jimbo la Njombe wakihojiwa na tume ya kuchunguza magogoro huo ambapo wananchi waliweka magogo kuziba barabara na kutaka kuchoma moto magari ya wawekezaji huku wakitishia kuvamia mashamba hayo. 

Kwa upande wao wawekezaji wa shamba la Ludodolelo wamesikitishwa na vurugu hizo huku Padre Arnord Likiliwike akisema kutaka kuchoma moto magari si dalili njema na lengo ni kujenga hivyo wanataka amani itawale katika kutatua mgogoro huo huku meneja wa shamba la Ludodolelo toka kampuni ya Silver lands Bw. Steven Maina akisema wao wameitwa kuzungumzia shamba hilo na kwamba nani wanapaswa kushikilia si hoja ya msingi kwao. 

Kaimu Mwenyekiti wa Tume ya kuchunguza mgogoro huo Bw.Joshua Ndyamukama ambaye pia ni Mkuu wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa(TAKUKURU) wilaya ya Makete amesema kuwa mwekezaji katika shamba la Ludodolelo kampuni ya Silver lands ilikuja bila kuripoti ofisi ya kijiji na kata


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo