Kaburi la Mtoto huyo anayedaiwa kuuawa kwa kipigo
Mei 31 mwaka huu mtoto wa miaka 17 alipigwa na watuhumiwa watatu katika kijiji cha Utweve kata ya Ukwama wilaya ya Makete mkoa wa Njombe akituhumiwa kuwa ni mwizi
Tukio hilo
linadaiwa kupelekea kifo cha mtoto huyo ambaye alifariki Juni 4 mwaka huu
akipatiwa matibabu Ikonda hospitali
Katika kijiji hicho kumekuwa na vikao vya mara kwa mara kufuatia watuhumiwa
wa mauaji hayo kupewa dhamana na mahakama baada ya kuonekana wanatuhuma za kuua
bila kukusudia
Ndugu mmoja wa marehemu amezungumza na Eddy Blog kwa dakika 54 kuelezea
jinsi ilivyokuwa mwanzo hadi mwisho, sikiliza sauti hapo chini:-
