Anayedaiwa Kuingiza Sh. Milioni 7 kwa Dakika Afikishwa Mahakamani

Mtuhumiwa Mohamed Yusuph Ally anayedaiwa kuingiza milioni 7 kwa dakika akipelekwa rumande.

MFANYABIASHARA anayedaiwa kukwepa kodi na kuingiza shilingi milioni 7 kwa dakika amesomewa mashitaka 199 leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar kisha kupelekwa rumande.

Mtuhumiwa huyo aitwaye Mohamed Yusuf Ally alisomewa mashitaka hayo likiwemo la kugushi na kuwasilisha taarifa za uongo kwa kamishna wa TRA akidaiwa fedha zaidi ya shilingi bilioni 15 za Kitanzania.
Watuhumiwa wakitolewa eneo la mahakama.

Mtuhumiwa huyo akiwa na wenzake watatu  hawakutakiwa kujibu chochote kwa sababu kesi hiyo ni ya uhujumu uchumi.

Hakimu aliyekuwa akisikiliza shauri hilo, Huruma Shaidi aliiahirisha na akasema itatajwa tena Julai 25 mwaka huu

Habari na picha: Denis Mtima


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo