Uchangiaji wa damu bado ni Ishu Makete (Audio)

Juni 14 Kila mwaka ni siku ya uchangiaji damu kwa hiyari inayoadhimishwa duniani kote kwa Lengo la upatikanaji wa damu salama itakayowasaidia wagonjwa wenye uhitaji ambao maisha yao yanategemea damu, imeelezwa kuwa mwitikio wa wananchi katika zoezi hilo wilayani Makete mkoani Njombe bado ni mdogo.

Akizungumza kwa njia ya simu na blog hii mganga mkuu wa wilaya ya Makete .Dr Joseph Gasper Kimaro amesema licha ya zoezi la uchangiaji wa damu salama kuanza tangu siku ya wauguzi duniani iliyofanyika Mei 12 mwaka huu, bado mwitikio ni mdogo kutoka kwa wachangiaji wa damu.

Amesema kuwa hali hiyo huwenda inatokana na kutofanywa uhamasishaji na utoaji wa elimu ya uchagiaji damu salama kwa wakazi wa wilaya ya Makete huku akisema hivi sasa wanatarajia kuanza kufanya hamasa ya uchangiaji wa damu salama kwa baadhi ya kata za wilaya ya Makete.

 
Dr. Kimaro amesema kuwa hakuna madhara kwa wanaochangia damu kama baadhi ya watu walivyoaminishwa  na kusema kuwa hivi sasa huduma hii inapatikana hospitali ya wilaya ya Makete.

Hata hivyo amewataka wananchi kutambua kuwa kila mmoja hajui siku ambapo atahitaji kuongezewa damu, hivyo ni vyema kushiriki kuchangia damu ambapo zoezi hilo kwa hospitali ya wilaya ya Makete linafanyika siku ya Jumatatu hadi Alhamisi kila wiki.



JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo