Kujitoa wafadhili kwaiathiri Makete, Leo kulikuwa na Mjadala

Serikali wilayani Makete mkoani Njombe imetakiwa kushirikiana na jamii kuhakikisha miradi mbalimbali inayofadhiliwa na wahisani na kutekelezwa katika wilaya hii kuhakikisha inaendelea kufanya kazi hata kama wafadhili hao watajitoa

Hayo yamesema hapo jana wilayani Makete katika kikao cha asasi isiyo ya kiserikali ya PADI kwa kushirikiana na wasaidizi wa kisheria wilaya ya makete MADIPASE na wadau mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha wasaidizi hao wa kisheria wanaendelea kufanya kazi zao wilayani Makete licha ya wafadhili wa mradi huo kufikia kikomo chao Desemba Mwaka huu

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Mh Egnatio Mtawa aliyeiwakilisha halmashauri yake katika kikao hicho amesema ni wakati wa jamii kutambua kuwa miradi yote yenye ufadhili, wafadhili wana mwisho wake hivyo ni wakati muafaka wa kuhakikisha wasaidizi hao wanaendelea kufanya kazi hata kama wafadhili wanajitoa

Amesema hawezi kutamka moja kwa moja katika kikao kicho kama halmashauri yake itatoa kitu gani kwa wasaidizi hao wa kisheria ikiwemo suala la usafiri, na badala yake wapeleke taarifa halmashauri na kupitia vikao halali majadiliano yatafanyika na yaliyopo ndani ya uwezo wa halmashauri yatatatuliwa
 Katibu wa MADIPASE akisoma taarifa

 Akiikabidhi meza kuu
 Bw Jackson kutoka PADI akiongea jambo
 Wageni waalikwa wakisikiliza
 Mh Mwandilava Diwani Kipagalo akichangia hoja
Mwenyekiti wa MADIPASE Mchungaji Sinene
 Meza kuu ikisikiliza jambo
 Wasaidizi wa kisheria Makete

 Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Mh Egnatio Mtawa







JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo