Askari akamatwa akipokea rushwa laivu huko Tanga, muone hapa

Jeshi la polisi mkoani Tanga linamshikilia aliyekuwa askari wake Bw Antoni Temu miaka 46 kwa tuhuma za kushawishi na kuchukua rushwa kutoka kwa dereva wa gari katika kijiji cha Kilumbo wilayani Handeni mkoani Tanga

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Tanga Zuberi Mwombeji askari huyo anachukuliwa hatua za kisheria na tayari ameshafukuzwa kazi na kwa sasa yupo mahabusu akisubiri kupelekwa mahakamani


Tukio hilo limetokea jana majira ya saa saba mchana kwenye eneo la barabara ya Segera - Chalinze, na leo asubuhi jeshi hilo limetangaza kuwa limemfukuza kazi na hatua za kisheria za kumfikisha mahakamani zinafanyika

Unaweza ukabonyeza play kumsikiliza kamanda wa polisi mkoani Tanga, Zuberi Mwombeji akizungumza kuhusiana na askari huyo kukamata na kukabidhiwa kwaTAKUKURU.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo