Serikali Wilayani Njombe Imewataka Wananchi Kuendelea Kudumisha Amani Katika Maeneo Yao Katika Kipindi Hiki Cha Kampeni za Uchaguzi Mkuu Pasipo Kusababisha Vurugu Katika Mikutano ya Kampeni.
Kauli Hiyo Imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba (pichani) Wakati Akizungumza na mtandao huu Ofisini Kwake Juu ya Mwenendo Mzuri wa Zoezi Kampeni Katika Wilaya ya Njombe.
Aidha Dumba Amesema Pamoja na Taifa Kuwa na Zoezi Kubwa na Muhimu la Uchaguzi Mkuu Hapo Oktoba 25 Mwaka Huu Lakini Bado na Mambo Mengine Yanakwenda Kadri Inavyowezekana.
Pamoja na Mambo Mengine Lakini Pia Amesema Wao Kama Viongozi Ndani ya Taifa la Tanzania Wanaendelea Kuhakikisha Amani na Utulivu Vinakuwepo Muda Wote Kwa Maslahi ya Watanzania Wote Hususani Wazee,Wanawake na Watoto Ambao Mara Nyingi Huwa ni Waathirika Wakubwa Katika Matatizo Mbalimbali.
Kwa Upande Wake Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe Lilisema Nalo Limejipanga Kikamilifu Ili Kuhakikisha Mchakato Huo Unakwenda Kama Ulivyopangwa Bila Kuingiliwa na Mtu Yeyote.