Saa chache baada ya kuripotiwa kifo cha Mchungaji Christopher Mtikila kilichotokea kwa ajali ya gari huko mkoani Pwani, uthibitisho wa kifo hicho umewekwa wazi na baadhi ya vyanzo sahihi
Wa kwanza ni kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Jafar Mohamed ambaye amesema ni kweli kifo hicho kimetokea kwa ajali ya gari kama alivyonukuliwa akizungumza na kituo cha televisheni cha ITV
Mtikila alikuwa ni mwenyekiti wa chama cha DP mpaka mauti yanamkuta leo asubuhi
