Vituo vya redio na TV zote nchini vyaonywa na TCRA

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imevitaka vituo vya redio na televisheni nchini Tanzania kuepuka kurusha habari za uchochezi hasa katika kipindi hiki cha kampeni kuelekea uchaguzi mkuu.
 Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dk. Ally Simba ameeleza kuwa  vyombo vya habari vinatakiwa kuepuka kurusha na kuandika habari zitakazochochea vurugu na uvunjifu wa amani kwan jamii ina imani kubwa na vyombo vya habari na waandishi wa habari, hivyo hawana budi kutumia weledi katika utoaji wa taarifa katika kipindi hiki cha kampeni kuelekea uchaguzi mkuu.


Radio 106 na televisheni 28, zimesajiliwa nchini Tanzaia na kwamba katika kuelekea uchaguzi mkuu, tayari vituo vitano vya televisheni vimekuwa na makosa yaliyosababisha kupewa adhabu na onyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo