Shamsa Ford: Nataka Mabadiliko.....Siwezi Kujidhalilisha Kufuata Fedha CCM


Staa wa  filamu ya Chausiku, Shamsa Ford amesema hatobadilisha msimamo wake wa kushabikia vyama vya upinzani kwa kulaghaiwa na wasanii wachache kwa maslahi yao binafsi .

Shamsa amesema hayupo tayari kufuata maamuzi ya watu wengine hata kwa lundo la fedha kwani  kufanya hivyo  ni kujidhalilisha .

“Mimi nitabaki huku kwa kuwa nahitaji mabadiliko,kila siku wasanii tunalia tukidai tunaibiwa na hakuna utekelezaji na matokeo yake tunapewa ahadi zisizoisha.”Amesema Shamsa

Aidha , Shamsa Ford aliwataka mashabiki kuwaona kama watu wakawaida kwani baada ya siasa maisha yataendelea kama zamani.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo