Mgombea Mwenza Samia Suluhu awaonya madereva bodaboda

Mgombea mwenza wa urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu, ameonya vijana waendesha bodaboda kuacha tabia ya kuwarubuni wanafunzi wa kike kwa chipsi na 'lifti' jambo linalowasababishia mimba zisizotarajiwa.
 
"Vijana ninyi na vipikipiki vyenu mnawaharibia maisha watoto wa kike kwa kuwapa mimba zisizotarajiwa," alisema Samia 
 
Kutokana na tatizo hilo, Samia alisema akichaguliwa yeye na mgombea wa urais kupitia CCM, Dk. John Magufuli atahakikisha anakabiliana na hali hiyo kwa kujenga mabweni ya wasichana katika shule za kata.
 
Alisema bila mabweni wasichana wa kike wataendelea kupata mimba zisizotarajiwa na hivyo kuharibu maisha yao.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo