Tikiti maji laleta maafa kwa familia jijini Dar es Salaam

Familia moja ya watu watano eneo la Migombani Tabata Segerea jijini Dar es Salaam imeugua ghafla baada ya kula tunda aina ya tikitimaji linalosadikiwa kuwa na sumu

Baba wa familia hiyo Alphonce Kiduko akielezea amesema baada ya kula tunda hilo hali ilianza kubadilika majira ya saa mbili usiku na kila aliyekula alianza kuumwa tumbo la kuhara

Amesema hali hiyo ilianzia kwake na baadaye kufuata kwa wanafamilia wengine ambapo baada ya muda wote walizidiwa na kulazimika kumpigia simu daktari

Wanafamilia wengine waliofikwa na mkasa huo ni Bariam Boniface na Anjelina Kiduko


Kwa upande wake muuguzi Blandina Charles ameelezea hatua walizochukua kwa wagonjwa hao baada ya kupewa taarifa kuwa ni pamoja na kuwatundikia madripu pamoja na kuwapa dawa za kunywa na mpaka sasa wanaendelea vizuri


Naye Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Migombani Japhet Kemba amekiri kuwa na taarifa ya familia hiyo kufikwa na mkasa huo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo