Huenda sasa Shilole anaweza kupata lepe la usingizi baada ya mwanasheria maarufu nchini, Albert Msando
kuahidi kumsaidia kufuatia kupewa adhabu kali na baraza la sanaa la taifa, BASATA hivi karibuni.
BASATA lilimfungia muimbaji huyo wa ‘Nakomaa na Jiji’ kutojihusisha na sanaa kwa mwaka mzima kutokana na
kitendo chake cha kuidhalilisha nchi alipokuwa akitumbuiza nchini Ubelgiji.
Shishi amepost selfie Instagram akiwa na Msando na kuandika, “Nakuheshimu my kaka umeweza kujitoa kwa ajir
yangu kwenye matatizo yangu! Mungu atakulipa inshaaalah @albertomsando.”
Bongo5 imempigia simu Shilole kutaka kupata maelezo ya ni kwa vipi mwanasheria huyo anamsaidia lakini amedai
kuwa yeye si mzungumzaji wa jambo hilo.
Msando ni mwanasheria wa watu wengi mashuhuri akiwemo Zitto Kabwe.
chanzo:bongo5