Rundo la Nyavu haramu zakamatwa na kuteketezwa ziwa Victoria

Serikali kupitia idara ya uvuvi mkoa wa mara imekamata na kuteketeza  kwa moto nyavu haramu za kuvulia samaki zenye thamani yazaidi ya shilingi milioni 98 baada ya kukutwa zitumika zikivua samaki ndani ya ziwa victoria kinyume cha Sheria.

Akizungumza kabla ya zoezi la uteketezaji wa nyavu hizo 3,285  kufanyika nje kidogo ya mji wa musoma,afisa mfawidhi wa usimamiziwa rasilimali za uvuvi kanda ya Mara Bw.Braison Meela,amesema nyavu hizo zimakamatwa katika operesheni  inayoendelea baada ya kukutwa zikitumika kuvua samaki katika wilaya za Butiama, Bunda,Musoma na Rorya mkoani Mara.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Musoma kamishina mwandamizi mstaafu wa jeshi la Polisi Zelothe Steven, pamoja na kupongeza juhudi hizo za kupambana na uvuvi huo haramu,lakini pia amataka operesheni hiyo kufanyika hadi katika  maduka yanayouza nyavu hizo,huku mkurugenzi mstaafu wa taasisi ya utafiti wa uvuvi  nchini Bw.Philip Bwathondi,akiwataka wanasiasa kuacha kufumbia macho uvuvi huo  haramu.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo