Jeshi la Polisi limesema limeshakamata bunduki 16 kati ya 21 zilizoporwa kwenye Kituo cha Stakishari.
Bunduki hizo ziliporwa Julai 12 wakati watu wanaoaminika kuwa ni majambazi walipovamia kituo hicho cha polisi, Ukonga – Dar es Salaam na kuua askari wanne na watu wengine watatu.
Jana, Naibu Kamishna wa Kanda ya Kipolisi ya Dar es Salaam, Simon Sirro aliwaambia waandishi wa habari kuwa zaidi ya majambazi 10 wameshakamatwa na polisi wanaendelea kuwahoji kuhusu tukio hilo.
“Silaha zilizokuwa zimebaki ni tano, 16 zimeshakamatwa na hizo tano ndizo tunafanya bidii ya kuzipata. Niwahakikishieni kuwa zitapatikana,” Sirro.
Alisema watuhumiwa waliovamia kituo hicho walikuwa zaidi ya 15 na walitumia mbinu mpya ambayo Polisi hawakuitegemea.
Wakati huohuo; Jeshi la Polisi limewakamata watu watatu kwa tuhuma za mauaji ya ofisa wa Polisi, Elibariki Palangyo yaliyotokea nyumbani kwake Yombo Kilakala, usiku wa Agosti.
Katika tukio jingine, polisi inawashikilia watu wanne wakituhumiwa kukutwa na vipande vinne vya meno ya tembo vyenye thamani ya Sh30 milioni juzi, saa 1.30 usiku huko Tandale kwa Mtogole.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi