Mwandishi wa habari Mkongwe apotea katika mazingira ya kutatanisha


Mzee Paul 
Sozigwa (pichani), aliyewahi kuwa Mwandishi wa Habari wa Rais katika serikali ya Awamu ya kwanza 
chini ya Mwalimu Nyerere, amepotea tangu jana mchana katika mazingira ya 
kitatanishi. 


Kwa mujibu wa taarifa ya familia yake ambayo Globu ya Jamii imeletewa, mara ya mwisho Mzee Sozigwa alionekana kanisani Mbezi Beach BCIC (kwa Gamanywa) jana
Jumapili saa nane mchana. Kupotea huku kunaleta mashaka hasa kwa kuwa Mzee Sozigwa ni mgonjwa wa
Alzheimer, na mara nyingi anapoteza kumbukumbu. Taarifa ya kupotea kwake
imeshatolewa polisi na kufunguliwa RB.


Taarifa hiyo imesema mara ya mwisho Mzee Sozigwa alikuwa amevaa shati 
jeupe lenye mistari ya bluu na kijivujivu, suruali nyeusi na viatu vyeusi.

Anapoulizwa anakaa wapi hujibu Kisarawe ama Vidunda, wilaya ya Kisarawe.

Atakayemuona anaombwa kupiga simu zifuatazo:

Mch. Moses Sozigwa  0712 3798180755 716158
Mrs. Irene Yussuf       0784 300418
Ms. Lucy Paul Sozigwa 0755 5640800717 310783
Mrs. Judith Mlawa      0712 834737

Unaweza pia kuwasiliana nao kwa Whatsapp na
Viber


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo